Wednesday, August 14, 2013

WATANZANIA TUMLINDE MWAKYEMBE MUNGU ANAKUSUDI NAYE KWETU

Kwamala nyingine tena wazili wa Uchukuzi Mh Dr. Harrison Mwakyembe a.ka JEMBE amevunja ukimya kwa kuamua kuchukua uamzi mgumu wa kushughurika na wauzaji wa madawa ya kulevya nchini. Mwakyembe ametoa siku 14 kuanzia jana na akaahidi kuwashughurikia kwa udi na uvumba watu wanaofanya biashara ya kuingiza na kuuza unga nchini. Akionyesha uwajibikaji leo Mwakyembe amefanya ziara ya kushitukiza katika uwanja wa ndege wa Mwalim J.K Nyerere ili kuongea na wafanyakazi na kujua nini kifanyike.

Mwakyembe amekua kiongozi wa mfano kwa kutofumbia macho maovu ambayo yanafanyika katika wizara yake katika kipindi chote ambacho amekua waziri. Itakumbukwa kuwa toka ateuliwe kuwa waziri wa uchukuzi mwakembe ameweza kushughurika na tatizo sugu katika bandari ya Dar es Salaam na kuondoa uozo na mizizi ya baadhi ya watumishi ambao walikuwa ni kikwazo cha ufanisi na utendaji kazi bandarini hapo. Tokea yafuanyike malekebisho hayo mapato ya bandari yameongezeka sanjari na ufanisi umeimalika kiasi cha kurudisha imani kwa watumiaji wa bandari hiyo.

                                          Waziri wa Uchukuzi DR. Harrison Mwakyembe

Wito wangu kwa watanzania wa dini zote na wasiokuwa na dini kumuombea Dr. Mwakyembe katika utendaji wake wa kazi hasa pale anapofanya kazi kwa masrahi ya taifa. Itakumbukwa kuwa viongozi wengi wameshindwa kupambana na vita hii kufuatia uwezo wa kifedha wa watu wanaofanya biashara hiyo kwa kuwa tayari kufanya lolote. Watanzania wenzangu ifike hatua tutambue kuwa ulinzi wa viongozi wawajibikaji uko mikononi mwetu hivyo ni vema tukajitoa muhanga kuwapigania kwa hari na mali.

Ni matumaini yangu kuwa tutampa ushirikiano wa kutosha muheshimiwa Mwakyembe katika kulisafisha taifa letu ambapo kwa sasa Tanzania imekuwa kinara wa uuzaji na usambazaji wa madawa ya kulevya. Sio hivyo tu pia inasadikika kuwa tayari mtambo wa kutengeneza dawa hizo upo nchini. Hongera sana Mwakyembe kwa kujitolea kumfunga paka kengele tuko nyuma yako.

Friday, August 9, 2013

SAKATA LA KUMWAGIWA TINDIKALI HALI NI TETE

Sakata la kumwagiwa tindikali mabinti wawili wa kiingereza ambao walikuwa wakijitolea huko Zanzibar rimechukua sura mpya baada ya watu mbalilmbali kutoa maoni ya kulaani tukio hilo. Wakitoa maoni yao kupitia mtandao wa skynews watu hao wamelaani na wengine kufikia hatua ya kumuomba waziri mkuu wa Uingereza kusitisha misaada kwa nchi ambazo ni tishio kwa raia wa nchi hiyo.



Akizungumza na skynews mama wa Kate Gee alisema kuwa mwanae ameungua sana na hivyo wanafanya jitihada kubwa ili aweze kulejeshwa nyumbani. Amesema familia kwa ujumla imesikitishwa sana na tukio hilo na kwasasa wanafanya uwezekano mtoto wao apate matibabu. tutaendelea kuwaletea taarifa zaidi kadri tunavyozipokea kutoka vyanzo vya habari vya uhakika

                                             Mama wa Kate Gee

HATUKUZIBA UFA SASA TUNAJENGA UKUTA LO!!!!!!

Naomba kuchukua muda wangu kuzungumza na watanzania wenzangu ila kabla sijaeleza mengi kwanza ningeomba kuuliza je hii ndio Tanzania tuitakayo? Je watanzania huyu pepo wa kuua na kudhuru watu ametoka wapi? Hivi karibuni kumekuwa na matukio mengi sana ya kuhudhunisha na kushitusha kwa watanzania wote. Ilianza kama mzaha pale ambapo kiongozi mmoja wa dini alipomwagiwa tindikari huko Zanzibar.

Kama mdhaha matukio ya watu kumwagiwa tindikali yakazidi kusambaa kwa kasi na hivi karibuni mfanya biashara maarufu hapa nchini ambaye anahusika na kuudha vifaa vya majumbani katika moja ya maduka maarufu hapa Dar alipomwagiwa tindikari. Yapo mengi ambayo yanasemwa baada ya matukio kama haya kutokea ambapo watu huyahusisha na mambo mbalimbali kama visasi na kadhalika

Kwa kuudhibitisha usemi usemao kuwa usipoziba ufa utajenga tabia hii imewakumba hata wageni ambao ni watu waliokuja kujitolea kufundisha watanzania bure bila malipo. Watanzia walistuka baada ta taalifa za mabinti wawili raia wa Uingereza Kate Geee na Kirstie Trup kumwagiwa tindikari na watu wasio julikana


Hivi hawa watu waliofanya hili tukio ni watanzania au ni maadui zetu wa kibiashara (utarii), nakama ni watanzania wanalengo gani na taifa letu? Je Tanzania yetu kwli imefika hapa tulipo kwa kuwashambulia watu ambao wamekuja hapa nchini kwetu kujitolea kufundisha watanzania? Mimi natoa wito kwa watanzania, vyombo vya usalama na serikali kwa ujumla kushikamana kuwafichua hawa wanaotaka kutia doa sekta ya utarii. Wenzetu wa Tanzania Zanzibar wanategemea sana utalii katika kuongeza kipato cha wazanzibali na serikali kwa ujumla.

Hebu tushikamane pamoja kuwafuchua hawa na ile tabia ya vyombo vya usallama na serikali kusema upelelezi unaendelea kisha mnakaa kimya utatufikisha pabaya kama taifa.

Thursday, April 4, 2013

Hivi Karibuni



Kumekuwa na mfumo wa vyama vingi tangu mwaka 1992 na tayari chaguzi zaidi ya mbili zimeshafanyika. Je kwa mtazamo wako unahisi mfumo wa vyama vingi unatusaidia katika kujenga umoja wa kitaifa na kuleta maendeleo katika nchi yetu? Hivi karibuni mungu akijaria nitafanya mazungumzo na baadhi ya wanasiasa mashuhuri hapa Tanzania. Ili watupe mtazamo na uzoefu wao na katika siasa za Tanzania. Kaa nami ni wakati wa vijana kutoa sauti na kujenga umoja wa kitaifa katika nchi yetu ili kusukuma gurudumu la maendeleo.

Wednesday, April 3, 2013

Happy Birthday Dr. Jane Goodall


I would like to take this chance to write this message to you as thanks for inspiring me in my life. I joined Roots & Shoots in 2000 when I was a student at Bulombora primary School in Kigoma. Then students selected me to be a president of Roots & Shoots at the school. That position helps me to learn on how to be a leader and to work with people. I traveled different places and meet with other young people who are Roots & Shoots members. I managed to have friends to all places which I visited, all this friends speaks one language and the language was (protecting people, animals and environment for the sustainable)….nice.

                                              Dr. Jane Goodall

In 2005 I started to volunteer at the Jane Goodall Institutes in Kigoma, I was operating in 26 Roots & Shoots clubs. From 2005 to 2007 I managed to increase Roots & Shoots clubs from 26 to 48 clubs. I like to volunteer because that it was a good time for me to learn about power of youth on making positive changes. When I was at the JGI-kigoma I met with a team from Pearson Foundation who teaches us to make public announcement and based calcium movies which helps we as members of Roots & Shoots to use make different movies to educate people about different problems facing them.


Isack Nyasilu (me) and my friend Jennifer Hudson during 2008 Jane Goodall Global Youth summit in Florida 

Thanks so much Dr. Jane Goodall for investing on youth and believing in youth, thanks for giving us power on solving and creating a huge family of people who love to care and protect people, animals and environment in general. I wish you happy birthday Jane Goodall
  


Friday, March 29, 2013

Muuwaji wa Padri Mushi Akamatwa



Jeshi la polisi Zanzibar linamshikilia mtu mmoja alietambulika kwa jina la Omar Mussa Makame kwa tuhuma za mauaji ya Padri Evarist Mushi wa Kanisa Katoliki Zanzibar yaliotokea  mwezi uliopita. Akizungumza na waandishi wa habari mjini Zanzibar Kamishna wa Polisi Zanzibar, Mussa Ali Mussa alisema kuwa kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo kumekuja baada ya kutolewa kwa picha yenye sura ya mtuhumiwa iliyochorwa na askari wa shirika la upelelezi la Marekani FBI.

Mtuhumiwa Omar Mussa Makame ambae ni mkazi wa  Mtaa wa Raha Leo mjini Zanzibar alikamatwa na kufanyiwa gwalide la utangulizi ambalo lilihusisha watu baadhi ambao walikuwepo siku ya tukio ambao walitambua sura ya mtuhumiwa. 

Akifafanua zaidi kamishina Mussa Ali Mussa alisema kuwa jeshi la polisi litampatia zawadi ya million kumi kwa siri mtu aliefanikisha kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo kama ilivyoahidi. Padri Evarist Mushi aliuwawa Februari 17 mwaka huu wakati akienda kuongoza ibada katika kanisa la Mtakatifu Teresia lililopo Beit el Raas mjini Zanzibar.

 Taswira ya mtuhumiwa wa mauaji ya Padri Mushi kama ilivyoandaliwa na FBI

Gari la marehemu Padri Mushi muda mfupi baada ya ya kuuwawa kwa kupigwa risasi

Gorofa laanguka Dar es salaam

Leo wakazi wa jiji la Dar es Salaam wameianza siku kwa majonzi makubwa baada ya taarifa za kuanguka kwa jengo la gorofa 16 katika eneo maarufu kwa msongamano wa watu na pilika pilika mbalimbali la kariakoo. Taarifa za awali zimemkariri Meya wa Ilala mheshimiwa Jerry Silaa kuwa maiti 2 zimepatikana na majeruhi 17. Pia muheshimiwa Silaa ameeleza kuwa Rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Jakaya Kikwete ameagiza vyombo vya ulinzi na usalama kusimamia zoezi la uokoaji na ulinzi wa mali za raia katika eneo hilo. YOUTH VOICE inaahidi kuwaletea habari kamili kadri zitakavyo kuwa zimapatikana na kuthibitiswa na vyombo vyenye mamlaka ya kutoa taarifa.

Tunapenda kutoa pole kwa watanzania wenzetu ambao wamewapoteza ndugu na marafiki zao, pia na wale waliopata majeraha wapone haraka. Pia tunaomba zoezi la uokoaji lifanyike kwa kasi na kwa uangalifu wa hari ya juu ili kuepusha madhara kwa watu ambao wanasadikika pengine wamefukiwa na kifusi hicho. Pia tunaomba hatua za kisheria zichukuliwe kwa wote ambao kwa namna moja ama nyingine walikwepa majukumu yao ama kwa kukusudia au kuto kukusudia na kusababisha jengo hilo kupolomoka. Tumechosha na hii tabia ya vifo kwa watanzania wasio kuwa na hatia ambavyo husababiswa na uzembe wa watu katika majukukmu yao




                           


                                       


Thursday, March 28, 2013

I'm back get prepared



Dear all
I’m sorry I have been out of response for almost five years this is due to many works which I have been doing. Now I’m back and I hope I will take my responsibility to give you out what young people the view through the window. So get prepared, thanks. By Isack 

Welcome to Youth Voice!

Follow this blog to hear from many different people every month. The youth of the world will send their views on politics, economics, society, the environment...anything! Tell us about what you've seen in the world. Tell us what you've heard. This blog will be for the youth to tell their stories from Alaska to Zanzibar!