Wednesday, August 14, 2013

WATANZANIA TUMLINDE MWAKYEMBE MUNGU ANAKUSUDI NAYE KWETU

Kwamala nyingine tena wazili wa Uchukuzi Mh Dr. Harrison Mwakyembe a.ka JEMBE amevunja ukimya kwa kuamua kuchukua uamzi mgumu wa kushughurika na wauzaji wa madawa ya kulevya nchini. Mwakyembe ametoa siku 14 kuanzia jana na akaahidi kuwashughurikia kwa udi na uvumba watu wanaofanya biashara ya kuingiza na kuuza unga nchini. Akionyesha uwajibikaji leo Mwakyembe amefanya ziara ya kushitukiza katika uwanja wa ndege wa Mwalim J.K Nyerere ili kuongea na wafanyakazi na kujua nini kifanyike.

Mwakyembe amekua kiongozi wa mfano kwa kutofumbia macho maovu ambayo yanafanyika katika wizara yake katika kipindi chote ambacho amekua waziri. Itakumbukwa kuwa toka ateuliwe kuwa waziri wa uchukuzi mwakembe ameweza kushughurika na tatizo sugu katika bandari ya Dar es Salaam na kuondoa uozo na mizizi ya baadhi ya watumishi ambao walikuwa ni kikwazo cha ufanisi na utendaji kazi bandarini hapo. Tokea yafuanyike malekebisho hayo mapato ya bandari yameongezeka sanjari na ufanisi umeimalika kiasi cha kurudisha imani kwa watumiaji wa bandari hiyo.

                                          Waziri wa Uchukuzi DR. Harrison Mwakyembe

Wito wangu kwa watanzania wa dini zote na wasiokuwa na dini kumuombea Dr. Mwakyembe katika utendaji wake wa kazi hasa pale anapofanya kazi kwa masrahi ya taifa. Itakumbukwa kuwa viongozi wengi wameshindwa kupambana na vita hii kufuatia uwezo wa kifedha wa watu wanaofanya biashara hiyo kwa kuwa tayari kufanya lolote. Watanzania wenzangu ifike hatua tutambue kuwa ulinzi wa viongozi wawajibikaji uko mikononi mwetu hivyo ni vema tukajitoa muhanga kuwapigania kwa hari na mali.

Ni matumaini yangu kuwa tutampa ushirikiano wa kutosha muheshimiwa Mwakyembe katika kulisafisha taifa letu ambapo kwa sasa Tanzania imekuwa kinara wa uuzaji na usambazaji wa madawa ya kulevya. Sio hivyo tu pia inasadikika kuwa tayari mtambo wa kutengeneza dawa hizo upo nchini. Hongera sana Mwakyembe kwa kujitolea kumfunga paka kengele tuko nyuma yako.

Friday, August 9, 2013

SAKATA LA KUMWAGIWA TINDIKALI HALI NI TETE

Sakata la kumwagiwa tindikali mabinti wawili wa kiingereza ambao walikuwa wakijitolea huko Zanzibar rimechukua sura mpya baada ya watu mbalilmbali kutoa maoni ya kulaani tukio hilo. Wakitoa maoni yao kupitia mtandao wa skynews watu hao wamelaani na wengine kufikia hatua ya kumuomba waziri mkuu wa Uingereza kusitisha misaada kwa nchi ambazo ni tishio kwa raia wa nchi hiyo.



Akizungumza na skynews mama wa Kate Gee alisema kuwa mwanae ameungua sana na hivyo wanafanya jitihada kubwa ili aweze kulejeshwa nyumbani. Amesema familia kwa ujumla imesikitishwa sana na tukio hilo na kwasasa wanafanya uwezekano mtoto wao apate matibabu. tutaendelea kuwaletea taarifa zaidi kadri tunavyozipokea kutoka vyanzo vya habari vya uhakika

                                             Mama wa Kate Gee

HATUKUZIBA UFA SASA TUNAJENGA UKUTA LO!!!!!!

Naomba kuchukua muda wangu kuzungumza na watanzania wenzangu ila kabla sijaeleza mengi kwanza ningeomba kuuliza je hii ndio Tanzania tuitakayo? Je watanzania huyu pepo wa kuua na kudhuru watu ametoka wapi? Hivi karibuni kumekuwa na matukio mengi sana ya kuhudhunisha na kushitusha kwa watanzania wote. Ilianza kama mzaha pale ambapo kiongozi mmoja wa dini alipomwagiwa tindikari huko Zanzibar.

Kama mdhaha matukio ya watu kumwagiwa tindikali yakazidi kusambaa kwa kasi na hivi karibuni mfanya biashara maarufu hapa nchini ambaye anahusika na kuudha vifaa vya majumbani katika moja ya maduka maarufu hapa Dar alipomwagiwa tindikari. Yapo mengi ambayo yanasemwa baada ya matukio kama haya kutokea ambapo watu huyahusisha na mambo mbalimbali kama visasi na kadhalika

Kwa kuudhibitisha usemi usemao kuwa usipoziba ufa utajenga tabia hii imewakumba hata wageni ambao ni watu waliokuja kujitolea kufundisha watanzania bure bila malipo. Watanzia walistuka baada ta taalifa za mabinti wawili raia wa Uingereza Kate Geee na Kirstie Trup kumwagiwa tindikari na watu wasio julikana


Hivi hawa watu waliofanya hili tukio ni watanzania au ni maadui zetu wa kibiashara (utarii), nakama ni watanzania wanalengo gani na taifa letu? Je Tanzania yetu kwli imefika hapa tulipo kwa kuwashambulia watu ambao wamekuja hapa nchini kwetu kujitolea kufundisha watanzania? Mimi natoa wito kwa watanzania, vyombo vya usalama na serikali kwa ujumla kushikamana kuwafichua hawa wanaotaka kutia doa sekta ya utarii. Wenzetu wa Tanzania Zanzibar wanategemea sana utalii katika kuongeza kipato cha wazanzibali na serikali kwa ujumla.

Hebu tushikamane pamoja kuwafuchua hawa na ile tabia ya vyombo vya usallama na serikali kusema upelelezi unaendelea kisha mnakaa kimya utatufikisha pabaya kama taifa.

Welcome to Youth Voice!

Follow this blog to hear from many different people every month. The youth of the world will send their views on politics, economics, society, the environment...anything! Tell us about what you've seen in the world. Tell us what you've heard. This blog will be for the youth to tell their stories from Alaska to Zanzibar!