Friday, March 29, 2013

Muuwaji wa Padri Mushi Akamatwa



Jeshi la polisi Zanzibar linamshikilia mtu mmoja alietambulika kwa jina la Omar Mussa Makame kwa tuhuma za mauaji ya Padri Evarist Mushi wa Kanisa Katoliki Zanzibar yaliotokea  mwezi uliopita. Akizungumza na waandishi wa habari mjini Zanzibar Kamishna wa Polisi Zanzibar, Mussa Ali Mussa alisema kuwa kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo kumekuja baada ya kutolewa kwa picha yenye sura ya mtuhumiwa iliyochorwa na askari wa shirika la upelelezi la Marekani FBI.

Mtuhumiwa Omar Mussa Makame ambae ni mkazi wa  Mtaa wa Raha Leo mjini Zanzibar alikamatwa na kufanyiwa gwalide la utangulizi ambalo lilihusisha watu baadhi ambao walikuwepo siku ya tukio ambao walitambua sura ya mtuhumiwa. 

Akifafanua zaidi kamishina Mussa Ali Mussa alisema kuwa jeshi la polisi litampatia zawadi ya million kumi kwa siri mtu aliefanikisha kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo kama ilivyoahidi. Padri Evarist Mushi aliuwawa Februari 17 mwaka huu wakati akienda kuongoza ibada katika kanisa la Mtakatifu Teresia lililopo Beit el Raas mjini Zanzibar.

 Taswira ya mtuhumiwa wa mauaji ya Padri Mushi kama ilivyoandaliwa na FBI

Gari la marehemu Padri Mushi muda mfupi baada ya ya kuuwawa kwa kupigwa risasi

No comments:

Post a Comment


Welcome to Youth Voice!

Follow this blog to hear from many different people every month. The youth of the world will send their views on politics, economics, society, the environment...anything! Tell us about what you've seen in the world. Tell us what you've heard. This blog will be for the youth to tell their stories from Alaska to Zanzibar!